Mama Salma
aeleza computer itakavyomuinua Mwanamke - March 13, 2010
Na Elizabeth Mtaja
Mke wa Raisi Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi
ya Wanaake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma, amesema teknolojia
ya komputya ina mchango mkubwa katika kuleta Maendeleo ya Wanawake
nchini .

Alitoa kauli hiyo jana alipopokea msada wa komputya 100 zenye
thamani ya dola za Marekani 60,000 zilizotolewa na kampuni ya
HUAWEI technology kutoka China, ikiwa ni mwendelezo wa Siku
ya Wanawake Duniani iliyoadhimishwa Machi 8 mwaka huu.
Matumizi ya komputya ni njia mojawapo ya kumuimarisha mwanamke
katika kujifunza na kujiimarisha katika biashara alisema
“Kwa kuwa WAMA inalenga kuboresha maisa ya Wanawake na watoto
hususan walio katika mazingira magumu naamini teknolojia hii
itaezesha kuboresha huduma zetu katika kumpatia mwanamke elimu
bora , huduma za afya na kumjengea uwzo kiuchumi”, alisema Mama
Salma.

Mama Salam alisema vitendea kazi hivyo walivyopokea vitatoa
mchango katika kuwajengea uwezo Wanawake katika shughuli za
Maendeleo na kuongeza kuwa ni matumaini kampuni ya HUAWEI itawekeza
zaidi nchini kupitia nyanja mbalimbali kwa ajili ya kuwanufaisha
wananchi wengi zaidi. Awali Mkurugenzi Mkuu wa HUAWEI Tanzania,
Yuan Song alisema mchango huo umetolewa kama njia mojawapo ya
kuunga mkono juhudi za Wanawake hapa nchini katika kujiletea
Maendeleo.
Komputya hizo zitagawiwa katika shule mbalimbali nchini na kipaumbele
kitatolewa kwa shule ya wasichana ikiwamo WAMA- NAKAYAMA iinayomilikiwa
na WAMA huko Nyamisati wilayani Rufiji.
|