..FOUNDATION NEWS

WAMA yasikitishwa na mimba , utoro shuleni, Machi 27 2010

Na Tabia Daffo, Babati

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete amesikitishwa na ukubwa wa tatizo la mimba na utoro kwa Wanafunzi wa mkoani Manyara.

Hali hiyo ilijitokeza baada ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Henry Shekifu, kumweleza Mama Salma kuwa tatizo la mimba na utoro limekuwa likirudisha nyuma Maendeleo ya sekta ya Elimu.

Mama Salma ambaye jana alitembelea na kuzungumza na Wanafunzi wa shule za masingi na sekondari Bonga wilayani hapa alielezwa kuwa kati ya Wanafunzi 1,155 walioachwa shule, 1097 ni watoro na 47 walipata mimba wakiwa shuleni.

Kufuatia hali hiyo Mama Salma aliwataka Wanafunzi kutumia fursa za Elimu wanazopata ili kutimiza malengo wanayojiwekea. Pia aliwataka kutambua wajibu mkubwa walionao katika kujipenda na kujilinda, ili kuhakikisha wanahitimu mafunzo na hatimaye kulitumikia taifa.

Site Search