..FOUNDATION NEWS

Mwenyekiti WAMA awashukia wanaume wanaokwepa kupima afya, Machi 27, 2010 Na Selina Wilson, Babati

Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), Mama Salma Kikwete amewacharukia wanaume wanaoshindwa kujitokeza kupima afya zao, hivyo kukwamisha mipango ya maendeleo.

Hilo linatokana na taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara , Henry Shekifu, kuwa asilimia 85 ya wanaojitokeza kupima virusi vya ukimwi ni wanawake, huku wanaume wakiwa asilimia 15 tu.

Baadhi yenu mnawakandimiza wanawake kwa kuwa tu nyinyi ni wanaume, basi onyesheni uanaume kwa kujitokeza kupima virusi vya ukimwi ilimjue afya zenu na mjipange kuishi kwa kujitambua, “ alisema”

Alisema kwa kujitokeza kwao kupima afya wanakwamisha mipango ya maendeleo, kwa kuwa kila mwaka hupangwa bajeti ya mahitaji ya dawa na vifaa kulingana na idadi ya wahitaji.

Mama Salma alisema kiwango cah maambukizi ya virusi vya ukimwi cah asilimia 1.6 mkoani Manyara kitakuwa si sahihi kwa kuwa wanaume wengi hawataki kupima afya zao.

Site Search