WAMA yawamwagia
mamilioni wanawake, Machi 28, 2010
Na Selina Wilson, Manyara
WANAWAKE mkoani Manyara wameendelea
kuneemeka kwa kuwezeshwa sh. Milioni saba toka Taasisi
ya Wanawake na Maendeleo (WAMA).
Fedha hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete
katika ziara yake ya siku mbili mkoani humo, kukagua shughuli
mbalimbali zikiwemo za ujasiriamali za wanawake.
Salma alikabidhi hundi ya sh. Millioni tatu kwa Umoja wa Wanawake
wa Tanzania (UWT) , mkoa wa Manyara. Kwa upande wa Wilaya ya
Mbulu alitoa hundi ya sh. Millioni nne kwa vikundi vinne vya
wanawake.

Akiwa wilayani Babati alikagua shughuli za bidhaa zinazotengenezwa
na wanachama wa UWT, ambapo mamia ya wanawake walikusanyika
katika ukumbi wa CCM wilayay hiyo na kumwonyesha bidhaa mbalimbali.
Akiwa Mbulu Mwenyekiti huyo wa WAMA alizindua utoaji mikopo
ya sh. 500,000/= kwa wanawake 95 Fedha hizo zilitolewa na WEDAC.
Akizungumza jitihada za ukombozi kwa wanawake , Salma aliwataka
kinamama kutotegemea mapato ya wanaume bali watafute kwao.
“Tusikae kusubiri kinababa mimi nilfundisha mpaka dakika ya
mwisho bial kuangalia uwaziri wa mume wangu niliacha baada ya
yeye kutangaza kuwania urais “
Aliwataka wanawake kushirikiana kusaka maendeleo na malezi
ya familia.
|