WAMA yachangia 1.5 ml. Kusaidia Timu ya Viziwi ya Mkoa wa Pwani kushiriki Michezo ya Kimataifa– Tumbi, Kibaha- Agosti 27, 2009
Mwenyekiti wa WAMA Mheshimiwa Mama Salma Kikwete amechangia shilingi millioni moja na laki tano kwa ajili ya kusaidia Timu ya Viziwi ya Pwani kushiriki kwenye michezo ya kimataifa wakati wa warsha ya ufunguzi wa Mkakati wa Kuendesha Michezo ya viziwi iliyofanyika wilayani Kibaha.
Akisoma risala kwa Mgeni rasmi Mwenyekiti Mstaafu wa Chama na Mweka hazina Klabu ya Michezo ya Viziwi Bw. Daudi Kulangwa amesema kuwa viziwi wanapenda sana michezo na wanaleta maombi kwa Mgeni rasmi ili wapatiwe viwanja vya michezo, vifaa, vitendea kazi vya ofisini na ushiriki wa michezo ya kimataifa. Walimweleza Mama Kikwete kuwa wanadaiwa shillingi millioni tatu. (3,000,000/=) kwa ajili ya ada ya usajili wa kimataifa ya shirikisho la viziwi duniani.

Mama Kikwete ambaye alikuwa Mgeni Rasmi kwenye warsha hiyo alisema amezielewa changamoto wanazokabiliana nazo na akahaidi kusaidiana nao pamoja na kuwapa nusu ya hela wanayodaiwa na akawomba na wadau wengi washirikiane kwa pamoja kutatua matatizo hayo.
Mama Kikwete pia aliikaribisha Timu ya viziwi kutermbelea mradi wa WAMA- wa Umoja wa Wakulima Hoyoyo, Mkuranga unaofanya kazi za Kilimo cha Paprika na Ufugaji wa Kuku wa Kienyeji na Mbuzi ulioko chini ya Kitengo cha Uwezeshwaji wa Wanawake.
Alieleza pia taasisi yake imekuwa ikiwasaidia watu wanoishi katika mazingira magumu kwa kupitia vitengo vyake vinne: Elimu, Afya, Uwezeshwaji wa Wanawake na Watoto Yatima na Wanaoishi Katika Mazingira Magumu.
|